MSANII wa filamu na muziki, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amefunguka kuwa kila akiandikwa kwa skendo mbaya, wanaye humsema na kumwambia hawataki kumuona akifanya hivyo tena.
Akistorisha na gazeti hili, Shilole kutokana na mkwara huo anaoupata kutoka kwa wanaye, Joyce na Rahma, amekuwa akijitahidi kuepukana na skendo mbaya ili asiwakwaze mara kwa mara.
“Ninawapenda sana wanangu na huwa wananisema sana hata kwa staili ninazocheza jukwaani ndiyo kazi inayoniwezesha kuwalea hivyo haina budi kunivumilia,” alisema Shilole.
>>GPL
About the Author

0 comments: