OMBI LA MAMA MAREHEMU SHARO MILIONEA KWA WAANDAJI WA MOVIE BONGO

5:05 AM - By Unknown 0


Ikiwa ni zaidi ya mwaka mmoja sasa tangu kufariki kwa Sharo Milionea,Mama mzazi wa Marehemu Sharo Milionea amekuja na ombi kwa ajili ya waandaaji wa Movie za kitanzania hapa nchini.
Ombi hili ni juu ya kazi mbalimbali alizowahi kufanya marehemu Sharo Milionea na hazikutoka enzi ya uhai wake ambapo mama ameomba kuzisimamisha kazi zote ambazo hazijatoka na marehemu Sharomilionea alishiriki,mpaka wawasiliane na familia hiyo.
Mama mzazi wa marehemu Sharo Milionea ameingia Dar es salaam jumapili,January 26 akitokea nyumbani kwake Kijiji cha Msanga wilaya ya Muheza Mkoa wa Tanga mahsusi kwa ajili ya kuipromote movie itakayoonyesha maisha ya Sharo Milionea.
Wahusika kwenye movie hiyo ni pamoja na Mama mzazi huyo pamoja na wanafamilia wa Sharo Milionea ambapo ndani ya movie hiyo ya maisha ya Sharo Milionea wameigiza tangu amezaliwa hadi alipofariki November 26 2012 kwenye ajali ya gari.
Bonyeza play kumsikiliza Mama mzazi wa Sharomilionea. 

Tags:
About the Author

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Pellentesque volutpat volutpat nibh nec posuere. Follow me @Bloggertheme9
View all posts by admin →

Get Updates

Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.

Share This Post

0 comments:

KABAMBE

© 2014 SWAGGA ZA BONGO. Distributed By MyBloggerThemes | Design By Bloggertheme9
Powered By Blogger.
back to top